Psalms 134

Wito Wa Kumsifu Mungu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)


1 aMsifuni Bwana, ninyi nyote watumishi wa Bwana,
ninyi mnaotumika usiku ndani ya nyumba ya Bwana.

2 bInueni mikono yenu katika pale patakatifu
na kumsifu Bwana.


3 cNaye Bwana, Muumba wa mbingu na dunia,
awabariki kutoka Sayuni.
Copyright information for SwhKC